Ugonjwa wa kisukari, kama jina linavyojieleza ni ongezeko la kiasi cha sukari katika damu. Ziko sababu nyingi zinazoweza sababisha ongezeko hili, ila kibaiologia ziko sababu mbili kubwa. nazo ni pamoja na mwili kushindwa kutengeneza insulin ya kutosha, au insulin inayotengenezwa kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Kazi moja wapo ya insulin ni kusaidia sukari itumike katika kutengeneza nguvu miilini mwetu. Hivyo tatizo lolote la homoni hii iitwayo insulin, huweza sababisha sukari kuongezeka katika damu. Katika lugha rahisi tunasema kwamba, sukari ikiwa nyingi katika damu inakuwa kama sumu. Sumu hii huleta matatizo mengi yakiwemo matatizo ya macho, pamoja na matatizo ya mishipa ya damu na fahamu, ambayo huweza kusababisha magonjwa ya moyo au kudhoofika kwa nguvu za kiume.
Yako matatizo chungu nzima yatokanayo na sukari kuzidi katika damu, na tutakuwa tukiongelea tatizo moja moja ili upate kuelewa vema. Ujumbe muhimu katika andiko hili, ni swala la kuzingatia udhibiti wa kiasi cha sukari katika damu. Kama wewe una ugonjwa wa kisukari, hakikisha unafuata masharti yote uliyoelekezwa na daktari wako ili kuzuia sukari isiongezeke sana katika damu. Kwa kufanya hivyo unaweza kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine. Kwa ushauri zaidi, usisite kuwasiliana nasi. Tuma maswali na maoni yako, na sisi tutakuwa tayari kabisa kukusaidia.
Yako matatizo chungu nzima yatokanayo na sukari kuzidi katika damu, na tutakuwa tukiongelea tatizo moja moja ili upate kuelewa vema. Ujumbe muhimu katika andiko hili, ni swala la kuzingatia udhibiti wa kiasi cha sukari katika damu. Kama wewe una ugonjwa wa kisukari, hakikisha unafuata masharti yote uliyoelekezwa na daktari wako ili kuzuia sukari isiongezeke sana katika damu. Kwa kufanya hivyo unaweza kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine. Kwa ushauri zaidi, usisite kuwasiliana nasi. Tuma maswali na maoni yako, na sisi tutakuwa tayari kabisa kukusaidia.


RSS Feed